Utafiti wa agizo la PK-12 la kuvaa barakoa
Kutokana na CDC kuidhinisha chanjo ya COVID-19 kwa watoto wa miaka 5 hadi 11 hivi maajuzi, agizo la PK-6 ya Idara ya Afya ya Kaunti ya Kent inayolazimu watu kuvaa barakoa inatarajiwa kuacha kutumika ndani ya siku 60. Baada ya hili kutokea, tunatarajia kuwa idara ya afya itapendekeza sana kuvaa barakoa wala si kufanya kuwa lazima.
Kulingana na maelezo haya, GRPS inataka kukusanya maoni kutoka kwa wanafunzi, wazazi/walezi wa wanafunzi wa GRPS na wafanyakazi wake ili kutathmini mtazamo wao wa ikiwa tunafaa kudumisha agizo la kuvaa barakoa la PK-12 au la. Tafadhali jibu maswali ya utafiti huu utakaokuchukua dakika 2. Majibu yote hayatatambulika kwa majina.