FOMU YA KUKUSANYA MAONI JUU YA UBORESHAJI WA MITAALA YA ELIMU
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Taasisi ya Elimu Tanzania imefungua jukwaa la wadau wa elimu kuhusu uboreshaji wa mitaala ya ElimuMsingi. Lengo kuu ni kupokea maoni ya wadau wa elimu yatakayosaidia kuboresha mitaala ya ngazi ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari nchini. Kama mdau wa Elimu unaombwa kutoa maoni yako kupitia fomu hii.