Utafiti wa Msingi wa Progamu ya Kimataifa ya Kufanya Mazingira Yote Yawe Salama

Mpendwa,

UNFPA inakushukuru kwa kushiriki katika utafiti huu mfupi. Utafiti huu ni sehemu muhimu ya Utafiti wa Msingi wa Programu ya  UNFPA inayoitwa  MASS. Programu ya MASS imeundwa kuziba mapengo yaliyopo katika programu zinazoshughulikia Ukatili wa Kijinsia unaowezeshwa na Teknolojia (TF GBV). Progamu hiyo inatekelezwa na Kitengo cha Ufundi cha UNFPA na Ofisi za Nchi za UNFPA huko Benin na Kenya, kuanzia Februari 2024 hadi Machi 2027. Progamu hiyo itashughulikia TF GBV kwa kutekeleza shughuli katika nguzo tano: Mwitikio, Kuzuia, Sheria na Sera, Utafiti na Tathmini, na juhudi za kuunganisha.

 Lengo la utafiti huu ni kutoa data ya msingi kwa ajili ya programu ya MASS. Ujumbe utakaopatikana kupitia utafiti huu mfupi utasaidia UNFPA kuelewa ufahamu na uzoefu wa watumiaji wa intaneti kuhusu TF GBV ambayo itatumika kufahamisha upangaji na utekelezaji wa programu ya MASS na itatumika kufuatilia na kutathmini matokeo ya programu.

 Majibu yote ni ya siri na na yatawekwa siri kabisa. Utafiti unatarajiwa kuchukua takriban dakika 10-15. Mwishoni mwa utafiti, utakuwa pia na nafasi ya kuongeza maoni mafupi ya ziada ambayo yanaweza kutoa taarifa zaidi na kutusaidia katika kuimarisha huduma za kuzuia na kukabiliana na TF GBV. Matokeo ya utafiti yatakuwa sehemu ya ripoti ya Utafiti wa Msingi ambayo itasambazwa na programu ya UNFPA ya MASS inayohusiana na kuweka mazingira yoye salama.

 Tunashukuru sana kwa ushiri wako muhimu. Ukipata swali lolote tafadhali wasiliana na timu ya utafiti wa msingi kwa: pdewi@unfpa.org. 

Kumbuka: Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) linafafanua TF GBV kama “kitendo cha unyanyasaji kinachofanywa na mtu mmoja au zaidi ambacho kinafanywa, kusaidiwa, kuchochewa na kukuzwa kwa sehemu au kikamilifu kwa matumizi ya teknolojia ya mawasiliano ya habari au vyombo vya habari vya digital, dhidi ya mtu kwa misingi ya jinsia zao.


Sign in to Google to save your progress. Learn more
Next
Clear form
Never submit passwords through Google Forms.
This form was created inside of United Nations Population Fund.

Does this form look suspicious? Report